JITAA
IMEANDIKWA NA
ERICK MACHUA
MUSICAL DRAMA
P.O.BOX
477
ARUSHA
TANZANIA
fade in
nje.jioni.barabarani
Watu wanaonekana wakiwa wenye haraka.Ni muda ambao watu
wametoka kwenye shughuli zao za siku (Rush hours)
(Sauti ya jitaa inasikika likipigwa taratibu)
cut to
nje.jioni.nyumbani kwa mr adam
Ni jumba kubwa la kifahari.Taa za nje zinaongeza uzuri wa
bungaloo hili.Getini gari linaingia taratibu.Taratibu linapaki kando ya magari
mengine ya kifahari.
(Sauti ya jitaa bado inasikika)
Mr Adam (59) anashuka kwenye gari akiwa amevalia suti nyeusi.Ni
mzee Mnene na Mrefu kiasi.Anaangalia huku na huko kisha anaelekea mlango wa
sebuleni.
cut to
ndani.jioni.nyumbani kwa mr adam.sebuleni
TV inawaka.Hakuna mtu sebuleni.Kwenye TV ni ya mziki inachezwa.
(Sauti ya jitaa bado inasikika.Inaingiliana na Sauti ya
mziki kwenye TV)
Mr Adam anatingisha kichwa kwa masikitiko.Anaelekea kwenye
kordo fupi.Sauti ya jitaa inasikika toka chumba kimojawapo.Anafungua mlango wa
chumba hicho.Ima (Emmanuel) (19) anaonekana amekaa juu ya kitanda akipiga jitaa
bila kufahamu baba yake anamuangalia kwa mlangoni.Mr Adam anafunga mlango na
kuelekea chumbani kwake.Ima anaacha kupiga jitaa baada ya kusikia kama mlango
wa chumbani kwake umeguswa.Anaangalia mlangoni.
cut to
ndani.jioni.chumbani kwa mr adam
Mrs Adam (56)anaonekana akipanga nguo kwenye kabati.Anageuka
baada ya mlango kufunguliwa na Mr Adam kuingia.Mr Adam anakaa kwenye kochi na
kuanza kufungua tai yake.
MR.ADAM
Umeshindaje?
mrs.adam
Salama, za kazi?
mr adam
Ah mambo yameenda vizuri ila wale jamaa wa Malawi ndo wanaonekana
hawako tayari.
mrs adam
Wana wasiwasi gani?
mr adam
Ah! hata nikikuelezea huwezi ukaelewa.ni complicated
kidogo…Anna hajafika bado?
MRS ADAM
Bado…ila atakuwa njiani
mr adam
Mbona imechukua muda hivyo?
mrs adam
Nilimuomba apitie kwa shangazi yangu aje na yule housegirl
mr adam
(kwa hasira kidogo)
Ah…hivi umeshakaa na Ima ukaongea nae?...mimi nikiongea nae
(continued)
CONTINUED:
nitakasirika tu..atanipandisha presha.
mrs adam
Baba Chriss..ni jana tu umeniambia niongee nae…leo nilikuwa
nashunguli nyingine sijaweza kukaa hata chini.
No comments:
Post a Comment