SHORT STORIES

-->
SAFARI YA MBUGANI.

Katika kusheherekea mahafali ya kumaliza chuo kikuu,marafiki sita waliamua kwenda kuweka kambi katika mbuga moja kama sehemu ya sherehe yao.Baada ya safari ya masaa kadhaa kutoka mjini walifika katika mbuga hiyo.Walitafuta sehemu nzuri na kuweka kambi yao.Walipoweka kambi palikuwa na bwawa dogo.Kwa mujibu wa taarifa walizopewa mapokezi nk kwamba wangeweza kuogelea katika bwawa hilo kwani halikuwa na hatari yoyote.Walitumia muda mwingi kuogelea na kucheza.Naam maji yalikuwa matamu na mazuri.

Jua lilipokuwa likiaga tayari walikuwa wamechoka hivyo walijipumzisha kwenye majani wakijikumbushia mambo mengi ya chuo.Hadithi zao nyingi zilikuwa za kufurahisha na kuchekesha.Mmmoja kati yao alipanda juu ya mwamba mkubwa uliokuwa karibu na bwawa na kujirusha kwenye maji wakati wengine wakiangalia.Vicheko vyao vilianza kufifia baada ya muda kupita bila rafiki yao kutoka ndani ya maji.Ghafla wakajirusha kwenye majani ili kumtafuta rafiki yao.Walitafuta kwa muda mrefu bila mafanikio.Hiyo ndo ilikuwa mwisho wa kumuona rafiki yo kipenzi.

Mwaka ulipita na  mioyo ikiwa imevunjika walirudi mbugani kwa ajili ya kuadhimisha kumbukumbu ya rafiki yao.Lakini walipokaribia bwawa walishtushwa  kumuona mtu kama rafiki yao.Alikuwa amesimama kando ya bwawa.Walisogea karibu.Fika alikuwa yeye.Walimuita lakini hakuitika.Walisogea karibu zaidi.Walipomkaribia  kwa namna ya ajabu na ya kustaajabisha hawakumuona mtu zaidi ya  mawimbi yakipepesa ndani ya maji.

No comments:

Post a Comment