Na Erick Machua
Alice’s
adventures in wonderland (Alice In Wonderland)ni Riwaya iliyoandikwa na
mwanariwaya maarufu wa kiingereza
Charles Lutwidge Dogson mwaka 1865.Ni hadithi inayomuelezea Binti
aitwaye Alice aliyedumbukia kwenye shimo la sungura na kujukuta akitokea katika
dunia nyingine ya ajabu na yenye viumbe visivyo vya kawaida.Ingawa Riwaya hii
imejijenga zaidi katika mambo ya kusadikika imejipatia umaarufu mkubwa sana
tangu ilipotolewa.Filamu mbalimbali zimepata kutolewa kutokana na Riwaya hii
maarufu zikiwa zile za Alice in Wonderland (1903
Alice's Adventures in Wonderland (1910
na nyingine nyingi.Umaarufu
wa kazi hii umepelekea kupatikana kwa msemo wa Alice in Wonderland.Msemo huu
hutumika sehemu mbalimbali kuashiria kitu cha ajabu ama kisichoeleweka. Kwa
mfano unaweza sema kwa kimombo “This-alice
-in wonderland economic system”yaani kumaanisha uchumi usioeleweka.Au
unaweza kusema kwa kwa Kiswahili rahisi “uchumi
wa nchi yetu ni kama Alice kwenye nchi ya ajabu”
No comments:
Post a Comment